Saturday, October 30, 2010

NDANI YA DAKIKA KUMI!!!

October 6, 2010
Inspired by real events...


Ndani ya Dakika kumi

Raha imeisha

Utamu umeondoka

Na ukweli umekuja

Hali halisi ya majuto.



Ndani ya dakika kumi,

Nimetoa nguvu zangu,

Nimemdhalilisha Mungu wangu

Nimeingia hasara kubwa,

Nimewapa sifa hawa mbwa!



Ndani ya dakika kumi

Sioni tena ile thamani 

Niliyokuwa nayo hapo zamani

Kubadili matukio natamani

Inaumiza moyo hii tafrani!!



Ndani ya dakika kumi

Ningeweza kusema hapana

Kuondokana na hii laana

Ningeweza tangaza msimamo

Kuchagua kuishi kama mfano



Ndani ya dakika kumi

Ningeweza zuia huu ujauzito

Nisingepitia haya mapito

Laiti mapema ningetiliia maanani 

Historia ingekua tofauti jamani



Ndani ya dakika kumi

Ningeishinda nafsi yangu

Ningeipa nguvu roho yangu

Ningemfurahisha Bwana wangu

Kwa kutotimiza starehe za hisia zangu



Ndani ya dakika kumi

Akili imenijia

Toba imenitawala

Najua mwili una muumba

Hilo halina mjadala



Ndani ya dakika kumi

Ninaamua kumpa nafasi

Yeye Mkuu aliyeamua kukaa nasi

Kwa nguvu zangu sitaweza

Nakiri yeye ndiye muweza



Ndani ya dakika kumi

Ninatambua sio uamuzi wa siku moja

Badiliko litachukua zaidi ya dakika kumi

Lakini mradi na Mungu tupo pamoja

Niko tayari aniongoze kila dakika kumi!

1 comment: